MASWALI
- Wewe ni gavana wa kaunti yako. Andika tawasifu utakayotoa katika sherehe ya kuapishwa kwako.
- Ugonjwa wa korona umeleta hasara nyingi kuliko faida nchini Kenya. Jadili.
- Mti mkuu ukigwa wana wa ndege huyumba.
- Andika insha itakayomalizika kwa maneno haya;
……………..nilisimama nikaangalia nyuma, machozi yakanitoka njia mbilimbili nilipokumbuka wosia wa wazazi na walimu.
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA INSHA
- SWALI LA KWANZA
- Hii ni insha ya kiuaminifu.
- Haya ni maandishi ya mtu binafsi kuhusu sifa zake maishani (mambo mazuri ya kutujengea sifa)
Mambo ya Kuzingatiwa- Mada – Ieleze anayetajwa katika tawasifu hiyo.
- Nafsi – Nafsi ya kwanza izingatiwe.
- Ijikite katika ujumbe kuhusu mtu binafsi yaani,
- Mwaka na mahali pa kuzaliwa.
- Aila/familia yake.
- Hali yake ya ndoa.
- Kiwango chake cha elimu – chuo kikuu, shule ya upili, ya msingi na ya chekechea.
- Vyeti na tuzo zote alizopata zitajwe.
- Matendo yake mema na mafanikio yatajwe ili aonekane kama kielelezo katika jamii.
- Aonyeshe tajriba yake katika kazi mbalimbali.
- Ni vyema aangazie juhudi zake maishani k.m amekuwa akijihusisha na shughuli zipi na amefaulu vipi, mipango yake kwa kaunti (Ruwaza yake)
- Ataje vipaji vyake mbalimbali;
Tashbihi; Kazi hii ipangwe kiaya na mawazo yafululize
- SWALI LA PILI
- Ni swali la mjadala.
- Mtahiniwa akubaliane na kauli kwa kutoa hoja nyingi za hasara na chache za faida
- Au mtahiniwa apinge kwa kutoa hoja nyingi za faida na chache za hasara.
- Atakayetoa hoja za faida pekee au za hasara pekee atakuwa amejibu swali nusu na asipate kiwango cha C.
Hasara - Vifo
- Shule kufungwa
- Kupoteza kazi
- Kafyuu
- Kusitishwa kwa usafiri.
- Visa vya wanafunzi kupachikwa mimba kuongezeka.
- Gharama ya maisha kupanda.
- Kadiria hoja zingine.
Faida - Wazazi kuwa na wanao kwa muda mwingi.
- Usafi kuzingatiwa na kuzuia ndwele k.v. kipindupindu.
- Biashara kuimarika – ya viyeyuzi, barakoa n.k.
- Masomo kuendelea kupitia mitandao.
- Kadiria hoja zingine.
- SWALI LA TATU
- Mti mkubwa huweka vitu vingi hasa ndege wanaojenga viota, kutaga na kuangua mayai yao pale. Ikiwa mti huo utaanguka makinda huumia kwa sababu wametegemea usalama wa mti huo.
- Mtu anayetegemea mtu mwingine kukidhi mahitaji yake hupata shida iwapo kifo au mtu huyo ataondolewa.
- Mtahiniwa athibitishe matumizi ya methali kwa kutoa kisa mwafaka.
- Mtahiniwa azingatie sehemu mbili za methali iwapo sivyo asipite Zaidi ya alama 10.
- SWALI LA NNE
- Mtahiniwa aandike kisa kinachomhusisha yeye akitenda makosa.
- Pawe na wasia/maonyo kutoka kwa wazazi na walimu.
- Akaidi wosia.
- Ajipate matatani na kujuta.
Join our whatsapp group for latest updates
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Butere Mock Exams 2021.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students