Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - KCSE 2021 Westlands Mock Exams

Share via Whatsapp

Maswali

MAAGIZO KWA MTAHINIWA

  • Andika insha mbili
  • Swali la kwanza ni la lazima
  • Kisha chagua insha nyingine moja kutoka kwa hizo tatu zilizo bakia.
  • Kila insha isipungue maneno 400.

 

  1. Swali la kwanza
    Wewe kama mwanahabari, umemtembelea Mkuu wa idara ya Trafiki nchini kujadili namna za kupunguza ajali barabarini. Andika Doyolojia hiyo. (alama 20)
  2. Jadili njia za kukabiliana na matatizo yanayokumba wanafunzi sheleni. (alama 20)
  3. Andika kisa kinachoafiki methali ifuatayo;
    Jino la pembeni halisitiri pengo. (alama 20)
  4. Andika kisa kinachomalizika kwa: Nilipoangalia jivu la nyumba yanga niligundua kuwa juhudi zangu za miaka mingi zilikuwa zimeungua zote. (alama 20)

Mwongozo wa Kusahihisha

  1. SWALI LA KWANZA
    Mwanafunzi aandike dayologia. Wahusika wote wawaili wazue hoja.
    Atakayechukua mkondo wa mahojiano atolewe 45.
    Makosa ya sarufi na hijai yaadhibiwe urefu wa maneno 400 uzingatiwe.

    Namna ya kupunguza ajali barabarani
    • Uanagalifu wa madereva.
    • Vidhibiti mwendo kwenye magari
    • Kuboresha/kukarabati barabara.
    • Kuchukulia hatua kali dereva walevi.
    • Kutoendesha gari kwa kasi
    • Kutotumia simu wanapoendesha magari.
    • Kuzingatia alama za barabarani.
    • Polisi fisadi wachukuliwe hatua kali
    • Madereva kupumzika kabla ya kuanza safari.
    • Ukaguzi wa magari kuhakikisha.
    • Kutobeba abiria au mizigo kupita kiasi.
    • Mtahini akadirie majibu ya mwanafunzi

  2. Njia za kukabiliana na matatizo yanayokumba wanafunzi shuleni.
    • Michezo shuleni
    • Ushauri nasaha.
    • Kuzungumza na wanafunzi wenzako/kujenga urafiki.
    • Kujiandaa kabla ya mtihani kwa kudurusu.
    • Kuchagua marafiki waandilifu.
    • Kuchagua masomo yanayolingana na uwezo wao.
    • Kutumia muda wao vizuri shuleni.
    • Kuchagua viranja wanaofaa.
    • Wasijilinganishe na wanafunzi wengi/wasijidharau.
    • Kuepuka uongo.
    • Kukamilisha kazi walizopewa kwa wakati ufaao.
    • Kudumisha heshima na nidhamu.
    • Kutumia muda waliotengewa kupumzika vizuri/kulalaa wakati waliotengewa.
    • Kuripoti kesi za wizi au hujuma yoyote ile.
  3. Jino la pembeni halisitiri pengo.
    • Mtu asiyekujua au usiye na uhusiano naye hawezi akakusaidia.
  4. Mwanafunzi arejelee kilichofanya nyumba yake iwe jivu. Aonyeshe jinsi aliweka juhudi na jinsi juhudi hizo ziliungua.
    • Mwanafunzi atakuayechukulia nyumba kijazanda kama ndoa, masomo atuzwe pia
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - KCSE 2021 Westlands Mock Exams.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest