- Utangulizi
- A-WA
- U-I
- U-YA
- YA-YA
- KI-VI
- LI-YA
- I-I
- I-ZI
- U-ZI
- U - U
- KU
- PAKUMU
- Jinsi Ngeli Mbalimbali Zinavyotumia: "a-nganifu", Viashiria na Viashiria Visisitizi.
- Virejeshi(-o, amba-), -enye, -enyewe, ote, o-ote, ingi, ingine n.k kulingana na ngeli mbalimbali.
Utangulizi
- Ngeli ni makundi ya nomino katika lugha ya Kiswahili yenye sifa zinazofanana kisarufi.
A-WA
- Huwa na majina ya watu, vilema, viumbe, vyeo na viumbe vya kiroho, n.k.
- Huchukua miundo kama vile M-WA, M-MI, KI-VI, n.k.
k.m.
- mtu - watu
- mkulima - Wakulima
- mtume - mitume
- mkizi - mikizi
- kiwete - viwete
- kibyongo - vibyongo
- nabii - manabii
- kuku - kuku
- waziri - mawaziri
U-I
- Huwa na majina ya mimea, sehemu za mwili, vifaa, matendo, maumbile, n.k.
- Mara mingi huchukua muundo wa M-MI.
k.m.
- mchungwa - michungwa
- mkoko - mikoko
- mkono - mikono
- mfupa - mifupa
- msumari - misumari
- mgomo - migomo
- msukosuko - misukosuko
- mlima - milima
- mwendo - myendo
- mwamba - myamba
U-YA
- Huwa na majina ya hali, matendo, n.k.
- Huchukua muundo wa U-MA.
k.m.
- Ugonjwa - magonjwa
- upana - mapana
- uasi - maasi
- uchungu - machungu
- ulezi - malezi
- uovu - maovu
- uhusiano - mahusiano
YA-YA
- Huwa na nomino zipatikanazo kwa wingi.
- Hazibadiliki katika umoja na wingi.
- Huchukua muundo wa MA-MA.
k.m.
- manukato
- mauti
- maziwa
- marashi
- mahubiri
- majira
- maradhi
- maafa
- mazingira
KI-VI
- Ni majina ya vifaa, sehemu za mwili, vitu, udogo, lugha, n.k.
- Huchukua miundo KI-VI na CH-VY.
k.m.
- kisu - visu
- kitabu - vitabu
- chakula - vyakula
- chanda - vyanda
- kijitu - vijitu
- kigombe - vigombe
- kiguu - viguu
- kidovu - vidovu
LI-YA
- Huwa na majina ya sehemu za mwili, dhana, vifaa, ukubwa, n.k.
- Huchukua muundo wa JI-MA, JI-ME, JA-MA, JE-MA n.k.
k.m.
- jicho - macho
- jina - majina
- jitu - majitu
- jino - meno
- goma - magoma
- jambo - mambo
- janga - majanga
- jembe - majembe
- jeneza - majeneza
- wazo - mawazo
- tunda - matunda
- jua - majua
- ziwa - maziwa
- ua-maua
I-I
- Huwa na nomino dhahania na vitu visivyoweza kuhesabika.
- Hazibadiliki katika umoja na wingi.
k.m.
- sukari
- amani
- chai
- mvua
- Imani
- chumvi
- subira
- imani
- amani
- furaha
I-ZI
- Huhusisha nomino dhahania na vitu.
- Hazibadiliki katika umoja na wingi.
k.m.
- nyumba
- baiskeli
- karatasi
- redio
- meza
- dini
- dawa
- ndizi
- jozi
U-ZI
- Huchukua miundo W-NY, U-NY, U-F, n.k.
k.m.
- wayo - nyayo
- wakati - nyakati
- uso - nyuso
- ufa - nyufa
- ufunguo - funguo
- ufagio - fagio
- wembe - nyembe
- uwanja - nyanja
- ujumbe - jumbe
- ukoo - koo
- waraka - nyaraka
- waya - nyaya
U - U
- Huwa na nomino za dhahania na vitu visivyoweza kuhesabika.
- Hazibadiliki kimaumbo.
- Huchukua U au W.
k.m.
- Ujinga
- Ulafi
- Ulaji
- Werevu
- Unga
- Uji
- Ugali
- udongo
KU
- Nomino zinazoundwa kutokana na vitenzi k.m. kuomba kwake kumemsaidia.
PAKUMU
- Ngeli ya mahali.
- Huwa na nomino moja ‘mahali’.
PA (mahali karibu au panapodhihirika) k.m. Kitabu kipo pale.
KU (mahali mbali au kusikodhihirika) k.m. Mahali kule kunafaa.
MU (ndani ya) k.m. Mahali mle mna siafu.
Jinsi Ngeli Mbalimbali Zinavyotumia: "a-nganifu", Viashiria na Viashiria Visisitizi.
NGELI | A-UNGANIFU | VIASHIRIA | VIASHIRIA VISISITIZI | ||||
KARIBU | MBALI KIDOGO | MBALI | KARIBU | MBALI KIDOGO | MBALI | ||
A-WA | wa | huyu | huyo | yule | yuyu huyu | yuyo huyo | yule yule |
wa | hawa | hao | wale | wawa hawa | ao hao | wale wale | |
KI-VI | cha | hiki | hicho | kile | kiki hiki | kicho hicho | kile kile |
vya | hivi | hivyo | vile | vivi hivi | vivyo hivyo | vile vile | |
LI-YA | la | hili | hilo | lile | lili hili | lilo hilo | lile lile |
ya | haya | hayo | yale | yaya haya | yayo hayo | yale yale | |
U-I | wa | huu | huo | ule | uu huu | uo huo | ule ule |
ya | hii | hiyo | ile | ii hii | iyo hiyo | ile ile | |
U-ZI | wa | huu | huo | ule | uu huu | uo huo | ule ule |
za | hizi | hizi | zile | zizi hizi | zizo hizo | zile zile | |
I-ZI | ya | hii | hiyo | ile | ii hii | iyo hiyo | ile ile |
za | hizi | hizo | zile | zizi hizi | zizo hizo | zile zile | |
U-YA | wa | huu | huo | ule | uu huu | uo huo | ule ule |
ya | haya | hayo | yale | yaya haya | yayo hayo | yale yale | |
YA-YA | ya | haya | hayo | yale | yaya haya | yayo hayo | yale yale |
I-I | ya | hii | hiyo | ile | ii hii | iyo hiyo | ile ile |
U-U | wa | huu | huo | ule | uu huu | uo huo | ule ule |
PA | pa | hapa | hapo | pale | papa hapa | papo hapo | pale pale |
KU | kwa | huku | huko | kule | kuku huku | kuko huko | kule kule |
MU | mwa | humu | humo | mle | mumu humu | mumo humo | mle mle |
Virejeshi(-o, amba-), -enye, -enyewe, ote, o-ote, ingi, ingine n.k kulingana na ngeli mbalimbali.
NGELI | VIREJESHI | -ENYE | -ENYEWE | -OTE | -O-OTE | -INGI | -INGINE | |
O-REJESHI | AMBA- | |||||||
A-WA | ye | ambaye | mwenye | mwenyewe | _ | yeyote | _ | mwengine |
o | ambao | wenye | wenyewe | wote | wowote | wengi | wengine | |
KI-VI | cho | ambacho | chenye | chenyewe | chote | chochote | kingi | kingine |
vyo | ambavyo | vyenye | vyenyewe | vyote | vyovyote | vingi | vingine | |
LI-YA | lo | ambalo | lenye | lenyewe | lote | lolote | jingi | jingine |
yo | ambayo | yenye | yenyewe | yote | yoyote | mengi | mengine | |
U-I | o | amabo | wenye | wenyewe | wote | wowote | mwingi | mwingine |
yo | amabayo | yenye | yenyewe | yote | yoyote | mingi | mingine | |
U-ZI | o | ambao | wenye | wenyewe | wote | wowote | mwingi | mwingine |
zo | ambazo | zenye | zenyewe | zote | zozote | nyingi | nyingine | |
I-ZI | yo | ambayo | yenye | yenyewe | yote | yoyote | nyingi | nyingine |
zo | ambazo | zenye | zenyewe | zote | zozote | nyingi | nyingine | |
U-YA | o | ambao | wenye | wenyewe | wote | wowote | mwingi | mwingine |
yo | ambayo | yenye | yenyewe | yote | yoyote | mengi | mengine | |
YA-YA | yo | ambayo | yenye | yenyewe | yote | yoyote | mengi | mengine |
I-I | yo | ambayo | yenye | yenyewe | yote | yoyote | nyingi | nyingine |
U-U | o | ambao | wenye | wenyewe | wote | wowote | mwingi | mwingine |
PA | po | ambapo | penye | penyewe | pote | popote | pengi | pengine |
KU | ko | ambako | kwenye | kwenyewe | kwote | kokote | kwingi | kwengine |
MU | no | ambamo | mwenye | mwenyewe | mwote | momote | mwingi | mwengine |
Download Ngeli za Kiswahili - Sarufi na Matumizi ya Lugha Kiswahili Notes.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students