MAAGIZO
- Andika insha mbili. Insha ya kwanza ni ya lazima.
- Kisha chagua insha moja nyingine kutoka hizo tatu zilizobakia
- Kila insha isipungue maneno 400
- Kila insha ina alama 20
- Wewe ni katibu wa chama cha waandishi habari chipukizi shuleni mwako. Andika kumbukumbu za mkutano uliofanyika mnamo MACHI 7, 2014.
- Fahali wawili wapiganapo ziumiazo ni nyasi.
- Anza kisa kwa maneno haya:
Mtoto aliletwa mbele yangu akiwa anatiririkwa damu usoni. Singeweza kumtambua hadi pale………………………………………………………. - Mvua husababisha madhara mengi. Jadili
Marking Scheme
- Hii ni insha ya kumbukumbu.
Ni muhimu mwanafunzi kufuata utaratibu wa uandishi wa insha ya kumbukumbu k.v- Lazima kuwe na anwani ya kumbukumbu
- Majina ya waliohudhuria
- Walituma udhuru
- Ajenda
- wasilisho la mwenyekiti.
- Kusomwa na kuthibitishwa kwa kumbukumbu za mkutano uliotangulia.
- Yatokanayo na kumbukumbu hizo.
- Kusajiliwa kwa wanchama wapya.
- Ziara ya wanchama.
- Usafi wa mazingira.
- N.k
(Watahini wahakiki ajenda za watahiniwa zikilenga mada na pia kufikia idadi inayohitajika) - Mambo mengineyo.
- Kufungwa kwa mkutano/kufunga mkutano.
- Kumbukumbu zenyewe. Kv.
- Kuwe na sehemu ya sahihi ya mwenyekiti pamoja na katibu wake (aliyeandika kumbukumbu hizo)
Mfano
Sahihi Tarehe
Katibu………………………………… …………………………….
Mwenyekiti …………………………. …………………………….
- Insha ya methali.
- Mtuhiniwa anaweza kuanza insha yake kwa kueleza maana ya methali au kuanza moja kwa moja kutoa kisa au visa.
- Sharti mtahiniwa asimulie kisa au visa kuthibitisha ukweli wa methali “Fahali wawili wapiganapo ziumiazo ni nyasi”
- Kisa au visa vilenge maana ya methali hii – wazozanapo viongozi/wakuu/wenye uwezo, wanyonge ndio huumia.
- Sharti kisa kilenge pande mbili za methali, jinsi, wenye uwezo walivyozozana na jinsi wanyonge walivyoahudhiwa na mzozo huo.
- Mtahinwa anayeshughulikia upande/sehemu moja ya swali au sehemu moja ya methali hajashughulikia swali kikamilifu na akadiriwe vilivyo. Asizoe alama zaidi ya C.
- Mtahiniwa aanze insha kwa maneno aliyopewa. Kisa chake kihusishe:
- Chanzo cha kuvuja damu.
- Uhusiano wa mwathiriwa na msimulizi.
- Usaidizi aliopewa mwathiriwa.
- Hatima ya tukio hilo.
Tanabahi: Mtahiniwa aliyeanza kisa kwa maneno tofauti, atakuwa amejitungia swali lake.
Kiwango chake ni D- ( 1 au 2 )
-
- Mwanafunzi anaweza kuzungumzia madhara na faida kisha atoe msimamo wake.
- Anaweza kuzungumzia madhara pekee pia.
Hoja
Madhara
- Mafuriko hutokea.
- Vifo vya watu na mifugo.
- Nyumba hubomoka.
- Huathiri usafiri – barabarani.
- Mimea huaharibiwa – huoza au hukosa kukua.
- Magonjwa hutokea k.m malaria kwa sababu ya mbu (hakuna masika yasiyo na mbu )
Faida
- Hukuza mimea / miti
- Mandhari huwa ya kupendeza.
- Chakula huwa kwa wingi.
- Maji ya kunywa / kutumia kwa viwanda n.k.
- Samaki na viumbe wa baharini
Join our whatsapp group for latest updates
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Form 3 Mid Term 1 Exams 2021.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students