Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Form 3 Mid Term 2 Exams 2021

Share via Whatsapp

MAAGIZO

  • Jibu Maswali yote
  • Swali la kwanza ni la lazima

Swali la lazima

  1. Andika dayalojia baina ya mtu na rafiki yake ambao ndiyo kwanza wakutane toka walipoachana katika shule ya msingi.
  2. Andika insha juu ya methali “Mti mkuu ukigwa wana wa nyuni huyumba”
  3. Kuboresha maisha katika magereza ni kukuza uhalifu. Jadili
  4. Niliskia jina langu likitajwa. Mmoja akaniita nikatoka nje. Nilisikia msongamano wa watu nyimbo za ushindi zikapanda juu!.................... Endeleza kisa hiki.


MARKING SCHEME

Makosa ya Sarufi

  1. Sahihisha kwa makini sana ukionyesha makosa yote yanayotokea. Makosa ya sarufi huwa
    Kuakifisha vibaya: Mifano, vikomo, vituo, alama ya kuuliza n.k.
  2. Kutumia herufi ndogo au kubwa mahali si pake.
  3. Matumizi mabaya ya ngeli na viambishi, nyakati, vihusiano, muundo mbaya wa sentensi na mnyambuliko wa vitenzi na majina.
  4. Kuacha au kuongeza maneno katika sentensi kwa mfano, „kwa kwa‟
  5. Matumizi ya herufi kubwa.
    Tazama: Matumizi ya herufi kubwa
    1. Mwanzo Wa sentensi.
    2. Majina ya pekee
    3. Majina ya mahali, miji, nchi n.k.
    4. Siku za juma, miezi ak.
    5. mashirika, masomo, vilabu u.k.
    6. Makabila, lugha u.k.
    7. Jina la Mungu.

Makosa ya Hijai/ tahajia
Haya ni makosa ya maendelezo. Sahihisha huka ukionyesha yanapotokea mara ya kwanza tu Makosa ya tahajia huwa katika:

  1. Kutenganisha maneno kama vile „aliye-kuwa‟
  2. Kuunganisha maneno kama vile „kwasabahu‟
  3. Kukata silabi vibaya kama vile „ngan-o‟
  4. Kuandika herufi inayofaa katika neno karna „mahari‟ badala ya mahali‟
  5. Kuacha herufi katika neno kama aliekuja badala ya aliyekuja.
  6. Kuongeza herufi isiyofaa katika neno kama piya badala ya pia
  7. Kuacha alama inayotarajiwa kuwepo katika herufi
  8. Kutoandika kistari cha kuunganisha neno ufikiapo pambizo au mwisho; au kuandika mahali si pake.
  9. Kuandika kistari pahali pasipofaa
  10. Kuacha ritifaa au kuiweka mahali pasipofaa.
  11. Kuandika maneno kwa ufupi mfano k.m nk, v.v

Mtindo
Mambo yatakayochunguzwa.

  1. Mpangiiio wa kazi kiaya.
  2. Mtiririko wa mawazo.
  3. Hati nzuri inayosomeka kwa urahisi.
  4. Namna anavyotumia methali, misemo, tamathali za usemi na mengineyo.
  5. Unadhifu wa kazi.
  6. Kuandika herufi vizuri k.rn: Jj, Pp, Uu, n.k.
  7. Sura ya insha.

Msamiati
Jumla ya maneno yaliyotumiwa kuafikiana na mada au kichwa kilichopendekezwa.

Swali la lazima

  1. Andika dayalojia baina ya mtu na rafiki yake ambao ndiyo kwanza wakutane toka walipoachana katika shule ya msingi.
    JIBU
    • Tanbihi: Dayalojia ni mazungumzo ya kawaida ya ‘nipe nikupe’ /fuata mtindo /mpangilio huu
    • Mtahiniwa abainishe wahusika kwa majina yao.
    • Semi koloni iwekwe baada ya jina la mhusika
    • Alama za usemi halisi zisitumiwe kamwe
    • Maelezo ya ziada yawekwe kwenye mabano
    • Viingizi/ vihisishi vitumiwe ili kuyapa mazungumzo uhalisia (uhai)
    • Mawazo yatiririshwe kwa namna inayoonyesha uhalisia
    • Mada tofauti zaweza kuzungumziwa.
  2. Andika insha juu ya methali “Mti mkuu ukigwa wana wa nyuni huyumba”
    Kugwa ni kuanguka: Nyuni ni ndege.
    • Methali ni mafumbo yenye maana fiche. Lazima mtahiniwa aguzie sehemu mbili za methali husika. Akiegemea upande mmoja aadhibiwe
    • Maana ya methali
      Mtu ambaye ndiye tegemeo la jamii au la mtu binafsi akiaga au aende asipatikane tena waliomtegemea wataumia.
    • Tanbihi
      Mtahiniwa aandike kisa au visa vinavyothibitisha ukweli wa methali hii.
  3. Kuboresha maisha katika magereza ni kukuza uhalifu. Jadili.
    • Hii ni insha ya mjadala: Mtahiniwa aweza kushughulikia upande wa kuunga pekee au ashughulikie upande wa kupinga pekee.
    • Mtahiniwa aweza kushughulikia pande zote mbili na kutoa uamuzi au msimamo wake
      HOJA: KUUNGA
      • Wafungwa wengine watakwepa majukumu
      • Si adhabu tena ikiwa wataishi raha mstarehe
      • Magereza yakiboreshwa watu watataka kuishi huko kukwepa majukumu yao
      • Watu wavivu watavunja sheria maksudi ili wawekwe korokoroni
      • Ukosefu wa usalama utafanya watu kukatalia gerezani
      • Si adhabu tena

        KUPINGA
      • Rekodi ya kuwa mfungwa humnyima mtu nafasi ya ajira katika viwango Fulani
      • Mtu huko kujiendeleza maishani
      • Mateso ya kifungoni ni makali kwa hivyo kifungo ni adhabu kubwa kwao.
      • Aibu ambayo hutokana na kuwa mfungwa humfanya mtu asipende kuishi gerezani.
  4. Niliskia jina langu likitajwa. Mmoja akaniita nikatoka nje. Nilisikia msongamano wa watu nyimbo za ushindi zikapanda juu!.................... Endeleza kisa hiki.
    • Hii ni insha ya mdokezo. Lazima mtahiniwa aendeleze kisa hiki wala asimalizie kwa mdokezo huu.
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Form 3 Mid Term 2 Exams 2021.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest