Kiswahili Questions and Answers - Form 3 Opener Term 1 Exams 2022

Share via Whatsapp

Maswali

INSHA (AL.20)
Mwandikie chifu wa sehemu unayotoka barua ukimjulisha juu ya mzazi katika kijiji chako anayewatesa na kuwanyima haki watoto wake.

MATUMIZI YA LUGHA (AL.30)

  1. Taja irabu mbili za kati. (AL.2)
  2. Taja konsonanti moja ya koromeo. ( AL.1)
  3. Eleza sifa tatu za kamusi .(al.3)
  4. Taja aina mbili za viambishi( Al.2)
  5. Eleza maana ya mofimu.(al.2)
  6. Taja matumizi mawili ya alama za italiki.(al.1)
  7. Eleza maana ya kielezi. (al.2)
  8. Tofoutisha maneno yafuatayo.(al.2)
    1. Dhamini
    2. Thamini
  9. Tumia kiulizi kifaacho kukamilisha maswali yafuatayo.(al.3)
    1. ………………wanitaniaa hivyo?
    2. ………………..ulienda kumwona?
    3. …………….Koko amewasilli?
  10. Tunga sentensi zinazokuwa na miundo ifuatayo. (al.3)
    1. N+T+N+E
    2. N+T
    3. N+V+T
  11. Andika ukubwa wa .(al.2)
    1. Mtoto
    2. Kikapu
  12. Eleza maana ya viwakilishi. (al.2)
  13. Kamilisha sentensi zifuatazo Kwa kutumia kirejeshi amba- (al.3)
    Tarishi…………………………..anayekuja ni mchezaji hodari
    Viazi…………………………… vimeliwa vilikuwa vimeiva.
    Nyufa …………………………. Zilizibwa jana zimebomoka.
  14. Tunga sentensi ukitumia vitenzi hivi katika hali ya kutendwa.(al.2)
    1. Vunja
    2. Funga

TAMTHILIA YA KIGOGO AL 20

  1. Fafanua ufaafu wa anwani kigogo. (al.10)
  2. …..Ni hilo embe lako,linanuka fee!
    1. Weka dondoo hili katika mktadha wake. (al.4)
    2. Taja tamathali ya usemi iliyotumika katika dondoo hili. (al.1)
    3. Taja sifa za msemewa. (al.5)

Mwongozo wa Kusahihisha

INSHA (AL.20)
Hii ni insha ya barua rasmi.
Lazima iwe na anwani mbili.

  • Anwani ya mwandishi
  • Tarehe
  • Anwani ya mwanikiwa
  • Mtajo
  • Mada
  • Maudhui
  • Sahihi

VIPENGELE VYA KUZINGATIA

  1. Kuwanyima elimu.
  2. Kuwanyima chakula.
  3. Kutowapa mavazi.
  4. Afya bora.
  5. Kuwafanyiza kazi nyingi.
  6. Uhuru wa kujiamlia.
  7. Kutowapa malazi.

MATUMIZI YA LUGHA (AL.30)

  1. Taja irabu mbili za kati. (AL.2)
    /a/ na /e /

  2. Taja konsonanti moja ya koromeo. ( AL.1)
    / h/

  3. Eleza sifa tatu za kamusi .(al.3)
    • Maneno yamepangwa kialfabeti
    • Huonyesha homonemia
    • Huonyesha mifano ya maneno mbalimbali

  4. Taja aina mbili ya viambishi( Al.2)
    • Viambishi awali
    • Viambishi tamati

  5. Eleza maana ya mofimu.(al.2)
    • Mofimu ni sehemu ndogo ya neno inayobeba maana kamili

  6. Taja matumizi mawili ya alama za italiki.(al.1)
    • Kuonyesha kiambishi cha kurejesha
    • Kuonyesha jina la kitabu
    • Kuonyesha maneno ya kigeni

  7. Eleza maana ya kielezi. (al.2)
    • Ni Kipashio katika sentensi kinachotumika kuelezea jinsi tendo linalotajwa na kitenzi lilivyofanyika.

  8. Tofoutisha maneno yafuatayo.(al.2)
    1. Dhamini-kuchukulia mtu dhamana ili mshtakiwa asiwekwe rumande
    2. Thamini-tia maanani ,heshimu

  9. Tumia kiulizi kifaacho kukamilisha maswali yafuatayo.(al.3)
    1. Mbona wanitaniaa hivyo?
    2. Je, ulienda kumwona?
    3. Je,koko amewasilli?

  10. Tunga sentensi zinazokuwa na miundo ifuatayo. (al.3)
    1. N+T+N+E
      • Mwanafunzi anasoma kitabu haraka
    2. N+T
      • Mwanafunzi anasoma
    3. N+V+T
      • Mtoto mtundu ameondoka

  11. Andika ukubwa wa .(al.2)
    1. Mtoto
      • toto
    2. Kikapu
      • kapu

  12. Eleza maana ya viwakilishi. (al.2)
    • Ni maneno yanayoleta dhana ya kuwa na kitu

  13. Kamilisha sentensi zifuatazo Kwa kutumia kirejeshi amba- (al.3)
    • Tarishi ambaye anayekuja ni mchezaji hodari
    • Viazi ambavyo vimeliwa vilikuwa vimeiva.
    • Nyufa ambazo Zilizibwa jana zimebomoka.

  14. Tunga sentensi ukitumia vitenzi hivi katika hali ya kutendwa.(al.2)
    1. Vunja
      • Musa alivunjwa mguu mpirani
    2. Funga
      • Mlango ulifungwa na mtoto

TAMTHILIA YA KIGOGO-MAJIBU AL.20

  1. Kigogo ni mtu mwenye madaraka makubwa kiutawala.
    • Majoka anatumia madaraka yake kulaghai wananchi.
    • Majoka anatangaza kipindi cha mwezi mzima cha kusherehekea uhuru.
    • Majoka anafunga soko la chapakazi ili ajenge hoteli ya kifahari.
    • Majoka anatumia mamlaka yake kumteka na kumtia ndani Ashua.
    • Majoka anapanga kutumia mamlaka yake kuzima uchunguzi wa Tunu kuhusu kifo cha Jabali.
    • Majoka anafuja pesa za kusafisha soko huku akijua hakuna wa kumhukumu kwa kuwa ndiye kiongozi.
    • Majoka anampa mamapima kibali cha kuuza pombe haramu kwa kutumia mamlaka yake.
    • Majoka anatumia mamlaka yake kudhibiti vyombo vya habari.
    • Majoka kwa mamlaka yake anaamuru polisi kutawanya waandamanaji.
    • Kwa mamlaka yake,Majoka anafadhili miradi isiyo muhimu.

  2.        
    1. Anayezungumza-Boza
      • Anayezungumziwa- Sudi
      • Mahali- katika karakana kwenye soko la Chapakazi
      • Tukio- walikuwa wakizungumza kuhusu uvundo ulioko kwenye mazingira
    2. Tanakali ya sauti-kunuka fee!
    3. Sudi
      • Ni mchonga kinyago
      • Ni mwenye bidii
      • Ni jasiri
      • Ni mwenye utu
      • Ni mkweli
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Form 3 Opener Term 1 Exams 2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest