Displaying items by tag: Sarufi

Mnyambuliko wa Vitenzi

Huku ni kuvibadili vitenzi kwa kurefusha viambishi tamati ili kuleta kauli mbalimbali Kauli hizi ni.

  • Tendana: uma - umana
  • Tendesha: lala – laza
  • Tendeka: Lima – limika

Huu ni upachikaji wa viambishi kwenye mzizi wa kitenzi ili kuunda vitenzi vipya

Kauli ya Kutendeshwa/Fanyisha

Huonyesha kuwa kitendo kimesababishwa na kitu Fulani

Vitenzi hivi hutambulishwa na vitenzi vya, za, sha, fya, na ,sa

Kauli ya Kutendata

Kauli hii huonyesha dhana ya kurudia rudia tendo
Mfano
Kata – katakata
Imba – imbaimba
Tia – tiatia
Ruka – rukaruka

Sifa Kutokana na Vitenzi

Ni kuunda maneno yenye kivumishi au kusifu nomino kutoka kwenye viarafa

Sifa hizi huwa ni herufi kama f, v, mw
Mfano
Amini – mwaminifu
Sikia- sikivu
Tii – tiifu
Dhulumu – dhalimu

Tanakali za Sauti

Ni maneno yanayoonyesha au kuiga milio ya sauti, hali Fulani, sura au vitendo mbalimbali. Hutumia kusisitiza namna vitendo vilivyo, vinavyotendeka au kitakavyotendeka

Mfano:

  • Funika gubigubi!
  • Papatika papatupapatu!
  • Kula fyu!
  • Kuregea regerege!

Matumizi ya Vihusishi ‘katika’ na Kiambishi Tamati –ni’

Katika na –ni ni vihusishi vinavyotumiwa kumaanisha ndani ya au kwenye

Vihusishi hivi havitumiwi pamoja katika sentensi

Mfano

  • Ingia katika darasani ni kosa
  • Ingia darasani au ingia katika darasa ni sahihi

-ni huambishwa kwenye nomino za kawaida kisha nomino hiyo huorodheshwa katika ngeli ya PAKUMU
Pia hutumika kuonyesha ndani ya au mahali ndani
Mfano
Vijiko vimo jikoni
Walimu wamo majilisini

Katika

  1. hutumiwa kuleta maana ya Miongoni mwa
    mtu mmoja katika wale ni mgonjwa
  2. Wakati
    Tutakuwa na likizo katika mwezi wa Aprili
  3. Ujumla wa vitu
    Wote walishiriki katika michezo hiyo

Alama za Uakifishaji

Ni alama zinazotumiwa ili kuwasilisha nia halisi na maana kamili ya kwenye maandishi

Alama hizi pia hufanya kusomeka kwa sentensi kuwa rahisi
Mfano

Nusukoloni /Semikoloni/Nukta kipumuo(;)

Hutumiwa kuunganisha mawazo mawili
Mfano
Ninataka kuondoka mapemasipendi kuchelewa

Koloni/Nuktambili/Nukta pacha (:)

Hutumiwa kuonyesha orodha ndefu
Mfano
Nenda ununue vutu vifuatavyo:maziwa, mkate, sukari, mafuta na chumvi

Ukubwa, Udogo na Wastani wa Nomino

Ukubwa ni hali ya kukuza nomino na udogo ni hali ya kudunisha nomino
Wastani ni hali ya kawaida ya nomino

Nomino katika ukubwa huwekwa katika ngeli ya LI – YA na nomino katika hali ya udogo huwekwa
katika ngeli ya KI – VI

Zipo kanuni ambazo hutumiwa

  • Nomino zenye silabi mbili- dodosha moja
    Mtu- jitu
  • Nomino zinazoanza kwa ki dondosha ki pachika ji
    Kiatu-jiatu

Kukanusha

Kukanusha Amri

Wakati wa amri hukanushwa kwa kutumia si
Mifano
Aende – asiende
Nimpe – nisimpe
Ule – usile

Swali lije baadaye
Wewe kunywa dawa
Wewe usikunywe dawa

Wingi na Kukanusha

Wakati wa sasa hukanushwa kwa ha
Mifano 

unasoma – mnasoma – hamsomi
unakula – mnakula – hamli

Vivumishi

Vivumishi vya Pekee Ingine na -O-ote

Vivumishi hivi ni ote, o-ote, enye, enyewe na ingine

Vitawe

Ni maneno yaliyo na maana zaidi ya moja
Mfano

  • Vua-toa samaki majini
            Toa nguo mwilini
  • Ala-aina ya mfuko ambamo kisu hufichwa
          Tamko la kushangaa
          Aina yoyote ya chombo cha kufanyia kazi 

Viwakilishi

Ni neno linalosimama badala ya nomino kama yeye, sisi, wewe

Ngeli na Viambishi Ngeli

Mifano ya ngeli:

  • A – WA
  • U – YA
  • I – ZI
  • U – U
  • YA – YA
  • I – I

Ngeli ya A- WA

Ngeli hii inahusisha majina yenye sifa na hali ya wanyama, nyuni, malaika, samaki na wanadamu

Kutoa mifano katika umoja na wingi
Mfano
Mnyoo – minyoo
Kiwete – viwete
Nzi – nzi
Mkunga – mikunga

Ngeli ya U – I

Nomino za ngeli hii huchukua upatanisho wa U katika umoja na I katika wingi
Mifano
Mkono – mikono
Muundi – miundi
Mzigo – mizigo
Mtaa – mitaa
Muhula – mihula
Mwaka – miaka
Mlingoti – milingoti

Ngeli ya KI – VI

Nomino za ngeli hii ni vitu vya kawaida

Majina huanza kwa ‘ki’ katika umoja na ‘vi’ katika wingi

Mengine huanza kwa ‘ch’ kwa umoja na ‘vy kwa wingi
Mifano
Kiazi – viazi
Kiatu – viatu
Kioo – vioo
Kina – vina
Kikuba – vikuba
Cheti – vyeti
Chakula – vyakula
Chanda – vyanda
Chungu – vyungu

Wastani            udogo
Mlango             kilango
Mguu                 kiguu

Ngeli ya LI – YA

Maneno katika ngeli hii huanza na ma, me

Maneno yote katika hali ya ukubwa huingizwa katika ngeli hii
Mifano 
Dirisha – madirisha
Embe – maembe
Zulia – mazulia

Ukubwa

Guu – maguu
Jibwa – majibwa

Ngeli ya U – YA

Maneno katika ngeli hii huanza kwa U katika umoja na Ya katika wingi
Mifano
Ugonjwa – magonjwa
Uuaji – mauaji
Ujazi - majazi
Upana - mapana

Ngeli ya YA – YA

Nomino zote huanzia kwa ma
Mifano
Masihara - masihara
Matatu-  matatu
Makazi - makazi
Mahakama - mahakama
Maakuli - maakuli
Mawasiliano - mawasiliano

Ngeli ya I – ZI

Nomino hazibadiliki katika umoja na wingi
Mifano
Mashine - mashine
Sinia - sinia
Sahani - sahani
Ngozi - ngozi
Taa - taa
Pete - pete
Sakafu - sakafu
Shingo - shingo

Ngeli ya U – ZI

Maneno katika ngeli hii huwa na upatanisho wa U na ZI katka wingi
Mifano
Ubeti – beti
Uchane – chane
Uchega – chega
Ubavu – mbavu
Ubao – mbao
Ulimi – ndimi
Udevu – ndevu
Ujari – njari
Ujiti – njiti
Ugoe – ngoe
Uzi – nyuzi
Ufa – nyufa
Waadhi – nyaadhi
Walio – nyalio
Waraka – nyaraka

Ngeli ya U – U

Huchukua U katika umoja na U katika wingi
Kuelezea maneno hayabadiliki katika umoja na wingi
Mifano
Moto - moto
Ugali - ugali
Wema - wema
Ufisadi - ufisadi
Wizi - wizi
Ubaya - ubaya
Uzembe - uzembe

Ngeli ya KU

Maneno katika ngeli hii huchukua upatanisho wa kisarufi KU

Ngeli ya I – I

Majina ya nomino hii huchukua upatanisho wa sarufi kuwa I katika umoja na I katika wingi

Ngeli ya PA KU MU

Ni ngeli ya mahali

Huelezea hali tatu

  • Hapa/hapo/pale- mahali dhahiri
  • Huku/huko/kule – kusiko dhahiri
  • Humo/humu/humo – mahali ndani

Kuelezea viambishi tofauti

Vihisishi

Kuelezea maana ya vihisishi
Hutumiwa kuonyesha hisi au hisia ya msemaji kidhihirisha

  • Furaha
  • Mshangao
  • Mshtuko
  • Hasira
  • Uchungu
  • Maumivu
  • Uchovu
  • Huruma
  • Dharau
  • Wito
  • Laana

Kutunga sentensi akitumia vihisishi alivyopatiwa

Vivumishi

Vivumishi ni maneno yanayotumiwa kuelezea zaidi kuhusu nomino

Aina za Vivumishi

  • A -Unganifu
  • Sifa
  • Pekee
  • Viulizi
  • Idadi
  • Vimilikishi
  • Viashiria

Viunganishi

Neno linalotumiwa kuunganisha neno na neno, sentensi na sentensi, wazo na wazo
Kutoa mifano tofauti ya viunganishi

  • Kasoro-lakini, bali
  • Kusalia kitu kimoja-ila, isipokuwa
  • Kinyume na matarajio-ingawa, ijapo, ilhali
  • Kulinganisha kuonyesha tofauti
  • Kuongezea-aidha, mbali na, licha ya
  • Kuwaongoza kutunga sentensi

A - Unganifu

Kijineno kinachotokana na kuambatanisha A na herufi tofauti kwa kutegemea ngeli

Jedwali
Ngeli                              A-unganifu
A – WA                          wa - wa
KI – VI                           cha - vya
LI – YA                           la - ya
U – I                              wa - ya
U – ZI                            wa- za
I – I                                ya - ya
U – U                             wa - wa
U – YA                           wa - ya
YA – YA                         ya - ya
I – ZI                             ya - zi
KU                                kwa - kwa
PAKUMU                      pa – pa , kwa – kwa, mwa - mwa

Mkato wa Maneno

Huhusu nomino pamoja na vimilikishi vyote vitatu
Mifano
Baba + yake = babake
Dada + yake =n dadake
Nyanya + yenu = nyanyenu
Shangazi + yake = shangaziye
Kaka + yako = kakako
Mjomba + yake = mjombake

Viulizi

Maneno yanayotumiwa kuuliza maswali
Mifano

  • Nani: hutumika katika ngeli ya A – WA kujua cheo, jina , ukoo wa watu
  • Nini: kujua ni kitu cha aina gani
    Hutumika katika ngeli zote isipokuwa ya A - WA
  • Gani:kujua aina , jamii, hali au tabia
  • Lini: kiulizi cha siku au wakati
    Hutumiwa kutaka kujua kipindi, siku au wakati wa tukio
  • Wapi:ni kiulizi cha mahali
  • Vipi:kiulizi cha namna gani
    Je ni neno la kuanzisha swali
  • Ngapi:kuuliza idadi kamili ya vitu , vyombo katika jumla
  • Pi: kubainisha kati ya nyingi ili kupata kihusika au mhusika Fulani mahususi

Vielezi

Neno linaloeleza jinsi kitendo kilivyotendeka au kufafanua zaidi kuhusu kitendo
Aina za vielezi

  • Wakati
  • Namna
  • Jinsi
  • Mahali
  • Idadi
  • Vuhusishi
  • Tanakali
  • Takriri
  • Tashbihi
    Hutumika kwa
  • Lini- wakati
  • Wapi – mahali
  • Vipi – jinsi au namna
  • Kiasi gani- idadi

Mifano
Wakati               mahali                          namna
Leo                   nyumbani                       taratibu
Kesho               darasani                       harakaharaka
Juma ijayo          Nairobi                         ghafla
Mtondogoo        machoni                        kivivu

Vielezi vya Mkazo

Takriri au shadda ni maneno yanayotumiwa kutilia mkazo au kusisitiza jambo
mifano ya takriri

  • salama salimini
  • bure bilashi
  • raha na buraha
  • kufa kupona
  • liwalo liwe
  • haambiliki hasemezeki
  • fanya juu chini
  • si wa uji si wa maji
  • daima dawamu
  • buheri wa afya
  • hakubali hakatai
  • hawashi hazimi

Ngeli pamoja Na Kirejeshi Amba

amba ni kitenzi kisaidizi kinachorejelea mtendwa au mtendaji kwa kutambulisha ama kueleza zaidi ya jambo fulani
kirejeshi –o hutumika badala ya AMBA
o-rejeshi na AMBA havitumiki pamoja
mfano
Kuku ambaye alitaga ni mkubwa

 Nomino     Ngeli    Amba-   o-rejeshi 
 Kuku

A-WA
KI-VI
LI-YA
U-I
I-ZI
U-ZI
I-I
U-U
U-YA
YA-YA
KU
PA
KU
MU

Ambaye-ambao 
Ambacho-ambavyo 
Ambalo-ambayo
Ambao-ambayo
Ambayo-ambazo
Ambao-ambazo
Ambayo-ambayo
Ambao-ambao
Ambao-ambayo
Ambayo-ambayo
Ambako
Ambapo
Ambako
Ambamo

 Ye-o
Cho-vyo
Lo-yo
O-yo
Yo-zo
O-zo
Yo-yo
O-oO
-yo Yo
-yo Ko

Po
Ko
MO

 

Kirejeshi –amba

Kirejeshi –o cha awali na kirejessho o- cha tamati
Kufafanua jinsi ya kuambisha o rejeshi tamati na awali
o-rejeshi awali hutokea kabla ya mzizi wa kitenzi –o- rejeshi tamati hutokea mwishoni mwa sentensi

 Kitenzi    o-rejeshi awali    o- rejeshi tamati 
Kimbia
Kula
Kuwa
Kua
Anayekimbia
Anayekula
Anayekuwa
Anayekua
 Akimbiaye
 Alaye
 Awaye
 Akuwaye

Matumizi ya –ndi

Kiainishi –ndi ni kishirikishi cha kukubali kwa msisitizo
Huambatanishwa na viwakilishi nafsi au virejeshi ili kutilia mkazo
Hutumia o-rejeshi kwenye vitenzi

Nafsi
Ndi + mimi = ndimi
Ndi + wewe = ndiwe
Ndi + yeye = ndiye
Ndi + si  = ndisi
Ndi + nyinyi  = ndinyi
Ndi + wao = ndio
o- rejeshi
ndi + ye = ndiye
ndi + o = ndio

Matumizi ya –si

Ni kiainishi cha kutilia mkazo

Huambatanishwa na viwakilishi nafsi au virejeshi ili kuleta msisitizo wa kukanusha
Nafsi
Si + mimi = simi
Si + wewe = siwe
Si + yeye  = siye
Si + sisi =  sisie
Si + wao = sio
o- Rejeshi
A –WA  si + yeye = siye     si + o = sio
KI – VI  si + cho = sicho     si+ vyo = sivyo

Matumizi ‘na’

Kiunganishi NA huambatanishwa na kiwakilishi nafsi kuonyesha PIA NA PAMOJA NA
Hutumiwa pamoja na 0-rejeshi
Nafsi
Ngeli               Na + o- rejeshi
A – WA            na+ye = naye nao
KI –VI              na + cho = nacho navyo
LI –YA              na + lo = nalo nayo
U – I                na + o = nao nayo
U – ZI              na + o = nao nazo
I – I                  na+ yo = nayo nayo
U – U               na + o = nao nao
U – YA             na + o= nao nayo
YA – YA            na +yo = nayo nayo
I – ZI                na + yo = nayo nazo
KU                   na + ko = nako 
PAKUMU         na+po  na+ko  na+mo

Matumizi ya ‘katika’, ‘ni’ , ‘kwenye’

Hivi ni vihusishi vya mahali
Hutumiwa kuonyesha kuwapo kwa kitu kilichotajwa mahali Fulani
Ngeli hubadilika hadi PA KU MU
Kuhimiza kuwa ni kosa kutumia hivi vihusishi pamoja
Kuambatanisha nomino na vivumishi

 Vivumishi   Darasa   darasani 
 Viashiria
 Vimilikishi 
 Ote
 Oote
 Enyewe
 Enye
 Ingine
 Sifa
Hili, hilo, lile 
Langu, lako,lake 
Lote
Lolote
Lenyewe
Lenye
Jingine
Zuri, jema, baya
Eupe, eusi
Halina

Hapa, hapo, pale 
Pangu, pako, pake 
Pote, kote, mote
Popote, kokote, momote
Penyewe, kwenyewe, mwenyewe 
Penye, kwenye, mwenye
Pengine, kwingine, mwingine
Pazuri, kuzuri, mzuri
Peusi, kweusi, mweusi
Hapana, hakuna, hamna

 

Usemi Halisi na Taarifa

Usemi halisi ni maneno yalivyotarajiwa na msemaji mwenyewe
Usemi taarifa ni ripoti au maelezo yakitolewa na mtu mwengine kutoka kwa msemaji halisi
Kueleza jinsi ya kubadilisha usemi
Usemi halisi                   usemi taarifa
leo                                   siku hiyo
Jana                                siku iliyopita/tangulia
Kesho                              siku ijayo
Viashiria hapa                 hapo au pale
Vimilikishi vya karibu       ake
Mbali kidogo                    ako
Nafsi ya kwanza              ni nafsi ya tatu
Wakati ta, ki                     nge

Mnyambuliko wa vitenzi

Kunyambua ni kurefusha mwisho wa vitenzi katika hali tofauti

  • Tendeka
  • Tendesha
  • Tendeshwa

Katika kauli ya kutendeka vitenzi humalizika kwa ‘ka’

Kitenzi                           kauli ya kutendeka
Vuka                              vukika
Sahau                            sahaulika
Maliza                            malizika
Bomoa                           bomoka
Kula                               kulika
Lala                                lalika
Lima                               limika
Pika                                pikika
Soma                             someka
Fagia                             fagilika

Kitenzi                         tendesha                    kauli ya kutendeshwa
Lala                                laza                           lazwa
Pika                                pikisha                      pikishwa
Kimbia                            kimbiza                     kimbizwa
Rudi                               rudisha                      rudishwa
Toa                                  toza                           tozwa
Ota                                 otesha                        oteshwa
Oa                                   oza                             ozwa
Soma                             somesha                    someshwa

Ukubwa na Udogo

Maneno katika hali ya ukubwa huwa ni kukipa kitu ukubwa usio wa kawaida na pia maneno katika hali ya udogo ni kukidunisha kitu kuliko hali ya kawaida
Ngeli pia hubadilika katika hali ya ukubwa na kuwa LI- YA ,na katika hali ya udogo huwa KI – VI
Njia tofauti za kubadili maneno katika ukubwa na udogo 
Kudodosha – mw, ny na kutia j
Mfano

  • ng’ombe – gombe
  • Mkono – kono
  • Ndama – dama

Kudodosha herufi moja na kutia ji
Mfano

  • Mji – jiji

Kudodosha ki na kutia ji
Mfano

  • Kisu – jisu

Kuongeza ji bila kudodoa chochote
Mfano

  • Jicho – jijicho

Kutia j kwa nomino zinazoanza kwa irabu
Mfano

  • uso – juso
  • Uta – juta