Displaying items by tag: Sarufi
Sarufi na Matumizi ya Lugha - Class 7 Kiswahili Revision Notes
- Mnyambuliko wa Vitenzi
- Tanakali za Sauti
- Matumizi ya Vihusishi ‘katika’ na Viambishi Tamati –ni’
- Alama za Uakifishaji
- Ukubwa, Udogo na Wastani wa Nomino
- Kukanusha
- Vivumishi
- Vitawe
- Viwakilishi
- Ngeli na Viambishi Ngeli
Mnyambuliko wa Vitenzi
Huku ni kuvibadili vitenzi kwa kurefusha viambishi tamati ili kuleta kauli mbalimbali Kauli hizi ni.
- Tendana: uma - umana
- Tendesha: lala – laza
- Tendeka: Lima – limika
Huu ni upachikaji wa viambishi kwenye mzizi wa kitenzi ili kuunda vitenzi vipya
Kauli ya Kutendeshwa/Fanyisha
Huonyesha kuwa kitendo kimesababishwa na kitu Fulani
Vitenzi hivi hutambulishwa na vitenzi vya, za, sha, fya, na ,sa
Kauli ya Kutendata
Kauli hii huonyesha dhana ya kurudia rudia tendo
Mfano
Kata – katakata
Imba – imbaimba
Tia – tiatia
Ruka – rukaruka
Sifa Kutokana na Vitenzi
Ni kuunda maneno yenye kivumishi au kusifu nomino kutoka kwenye viarafa
Sifa hizi huwa ni herufi kama f, v, mw
Mfano
Amini – mwaminifu
Sikia- sikivu
Tii – tiifu
Dhulumu – dhalimu
Tanakali za Sauti
Ni maneno yanayoonyesha au kuiga milio ya sauti, hali Fulani, sura au vitendo mbalimbali. Hutumia kusisitiza namna vitendo vilivyo, vinavyotendeka au kitakavyotendeka
Mfano:
- Funika gubigubi!
- Papatika papatupapatu!
- Kula fyu!
- Kuregea regerege!
Matumizi ya Vihusishi ‘katika’ na Kiambishi Tamati –ni’
Katika na –ni ni vihusishi vinavyotumiwa kumaanisha ndani ya au kwenye
Vihusishi hivi havitumiwi pamoja katika sentensi
Mfano
- Ingia katika darasani ni kosa
- Ingia darasani au ingia katika darasa ni sahihi
-ni huambishwa kwenye nomino za kawaida kisha nomino hiyo huorodheshwa katika ngeli ya PAKUMU
Pia hutumika kuonyesha ndani ya au mahali ndani
Mfano
Vijiko vimo jikoni
Walimu wamo majilisini
Katika
- hutumiwa kuleta maana ya Miongoni mwa
mtu mmoja katika wale ni mgonjwa - Wakati
Tutakuwa na likizo katika mwezi wa Aprili - Ujumla wa vitu
Wote walishiriki katika michezo hiyo
Alama za Uakifishaji
Ni alama zinazotumiwa ili kuwasilisha nia halisi na maana kamili ya kwenye maandishi
Alama hizi pia hufanya kusomeka kwa sentensi kuwa rahisi
Mfano
Nusukoloni /Semikoloni/Nukta kipumuo(;)
Hutumiwa kuunganisha mawazo mawili
Mfano
Ninataka kuondoka mapema; sipendi kuchelewa
Koloni/Nuktambili/Nukta pacha (:)
Hutumiwa kuonyesha orodha ndefu
Mfano
Nenda ununue vutu vifuatavyo:maziwa, mkate, sukari, mafuta na chumvi
Ukubwa, Udogo na Wastani wa Nomino
Ukubwa ni hali ya kukuza nomino na udogo ni hali ya kudunisha nomino
Wastani ni hali ya kawaida ya nomino
Nomino katika ukubwa huwekwa katika ngeli ya LI – YA na nomino katika hali ya udogo huwekwa
katika ngeli ya KI – VI
Zipo kanuni ambazo hutumiwa
- Nomino zenye silabi mbili- dodosha moja
Mtu- jitu - Nomino zinazoanza kwa ki dondosha ki pachika ji
Kiatu-jiatu
Kukanusha
Kukanusha Amri
Wakati wa amri hukanushwa kwa kutumia si
Mifano
Aende – asiende
Nimpe – nisimpe
Ule – usile
Swali lije baadaye
Wewe kunywa dawa
Wewe usikunywe dawa
Wingi na Kukanusha
Wakati wa sasa hukanushwa kwa ha
Mifano
unasoma – mnasoma – hamsomi
unakula – mnakula – hamli
Vivumishi
Vivumishi vya Pekee Ingine na -O-ote
Vivumishi hivi ni ote, o-ote, enye, enyewe na ingine
Vitawe
Ni maneno yaliyo na maana zaidi ya moja
Mfano
- Vua-toa samaki majini
Toa nguo mwilini - Ala-aina ya mfuko ambamo kisu hufichwa
Tamko la kushangaa
Aina yoyote ya chombo cha kufanyia kazi
Viwakilishi
Ni neno linalosimama badala ya nomino kama yeye, sisi, wewe
Ngeli na Viambishi Ngeli
Mifano ya ngeli:
- A – WA
- U – YA
- I – ZI
- U – U
- YA – YA
- I – I
Ngeli ya A- WA
Ngeli hii inahusisha majina yenye sifa na hali ya wanyama, nyuni, malaika, samaki na wanadamu
Kutoa mifano katika umoja na wingi
Mfano
Mnyoo – minyoo
Kiwete – viwete
Nzi – nzi
Mkunga – mikunga
Ngeli ya U – I
Nomino za ngeli hii huchukua upatanisho wa U katika umoja na I katika wingi
Mifano
Mkono – mikono
Muundi – miundi
Mzigo – mizigo
Mtaa – mitaa
Muhula – mihula
Mwaka – miaka
Mlingoti – milingoti
Ngeli ya KI – VI
Nomino za ngeli hii ni vitu vya kawaida
Majina huanza kwa ‘ki’ katika umoja na ‘vi’ katika wingi
Mengine huanza kwa ‘ch’ kwa umoja na ‘vy kwa wingi
Mifano
Kiazi – viazi
Kiatu – viatu
Kioo – vioo
Kina – vina
Kikuba – vikuba
Cheti – vyeti
Chakula – vyakula
Chanda – vyanda
Chungu – vyungu
Wastani udogo
Mlango kilango
Mguu kiguu
Ngeli ya LI – YA
Maneno katika ngeli hii huanza na ma, me
Maneno yote katika hali ya ukubwa huingizwa katika ngeli hii
Mifano
Dirisha – madirisha
Embe – maembe
Zulia – mazulia
Ukubwa
Guu – maguu
Jibwa – majibwa
Ngeli ya U – YA
Maneno katika ngeli hii huanza kwa U katika umoja na Ya katika wingi
Mifano
Ugonjwa – magonjwa
Uuaji – mauaji
Ujazi - majazi
Upana - mapana
Ngeli ya YA – YA
Nomino zote huanzia kwa ma
Mifano
Masihara - masihara
Matatu- matatu
Makazi - makazi
Mahakama - mahakama
Maakuli - maakuli
Mawasiliano - mawasiliano
Ngeli ya I – ZI
Nomino hazibadiliki katika umoja na wingi
Mifano
Mashine - mashine
Sinia - sinia
Sahani - sahani
Ngozi - ngozi
Taa - taa
Pete - pete
Sakafu - sakafu
Shingo - shingo
Ngeli ya U – ZI
Maneno katika ngeli hii huwa na upatanisho wa U na ZI katka wingi
Mifano
Ubeti – beti
Uchane – chane
Uchega – chega
Ubavu – mbavu
Ubao – mbao
Ulimi – ndimi
Udevu – ndevu
Ujari – njari
Ujiti – njiti
Ugoe – ngoe
Uzi – nyuzi
Ufa – nyufa
Waadhi – nyaadhi
Walio – nyalio
Waraka – nyaraka
Ngeli ya U – U
Huchukua U katika umoja na U katika wingi
Kuelezea maneno hayabadiliki katika umoja na wingi
Mifano
Moto - moto
Ugali - ugali
Wema - wema
Ufisadi - ufisadi
Wizi - wizi
Ubaya - ubaya
Uzembe - uzembe
Ngeli ya KU
Maneno katika ngeli hii huchukua upatanisho wa kisarufi KU
Ngeli ya I – I
Majina ya nomino hii huchukua upatanisho wa sarufi kuwa I katika umoja na I katika wingi
Ngeli ya PA KU MU
Ni ngeli ya mahali
Huelezea hali tatu
- Hapa/hapo/pale- mahali dhahiri
- Huku/huko/kule – kusiko dhahiri
- Humo/humu/humo – mahali ndani
Kuelezea viambishi tofauti
Sarufi na Matumizi ya Lugha - Class 8 Kiswahili Revision Notes
- Vihisishi
- Vivumishi
- Viunganishi
- Viulizi
- Vielezi
- Ngeli pamoja Na Kirejeshi Amba
- Kirejeshi-amba
- Matumizi ya -ndi
- Matumizi ya -si
- Matumizi ya Na
- Matumizi ya katika, Ni, kwenye
- Usemi Halisi na Taarifa
- Mnyambuliko wa vitenzi
- Ukubwa na Udogo
Vihisishi
Kuelezea maana ya vihisishi
Hutumiwa kuonyesha hisi au hisia ya msemaji kidhihirisha
- Furaha
- Mshangao
- Mshtuko
- Hasira
- Uchungu
- Maumivu
- Uchovu
- Huruma
- Dharau
- Wito
- Laana
Kutunga sentensi akitumia vihisishi alivyopatiwa
Vivumishi
Vivumishi ni maneno yanayotumiwa kuelezea zaidi kuhusu nomino
Aina za Vivumishi
- A -Unganifu
- Sifa
- Pekee
- Viulizi
- Idadi
- Vimilikishi
- Viashiria
Viunganishi
Neno linalotumiwa kuunganisha neno na neno, sentensi na sentensi, wazo na wazo
Kutoa mifano tofauti ya viunganishi
- Kasoro-lakini, bali
- Kusalia kitu kimoja-ila, isipokuwa
- Kinyume na matarajio-ingawa, ijapo, ilhali
- Kulinganisha kuonyesha tofauti
- Kuongezea-aidha, mbali na, licha ya
- Kuwaongoza kutunga sentensi
A - Unganifu
Kijineno kinachotokana na kuambatanisha A na herufi tofauti kwa kutegemea ngeli
Jedwali
Ngeli A-unganifu
A – WA wa - wa
KI – VI cha - vya
LI – YA la - ya
U – I wa - ya
U – ZI wa- za
I – I ya - ya
U – U wa - wa
U – YA wa - ya
YA – YA ya - ya
I – ZI ya - zi
KU kwa - kwa
PAKUMU pa – pa , kwa – kwa, mwa - mwa
Mkato wa Maneno
Huhusu nomino pamoja na vimilikishi vyote vitatu
Mifano
Baba + yake = babake
Dada + yake =n dadake
Nyanya + yenu = nyanyenu
Shangazi + yake = shangaziye
Kaka + yako = kakako
Mjomba + yake = mjombake
Viulizi
Maneno yanayotumiwa kuuliza maswali
Mifano
- Nani: hutumika katika ngeli ya A – WA kujua cheo, jina , ukoo wa watu
- Nini: kujua ni kitu cha aina gani
Hutumika katika ngeli zote isipokuwa ya A - WA - Gani:kujua aina , jamii, hali au tabia
- Lini: kiulizi cha siku au wakati
Hutumiwa kutaka kujua kipindi, siku au wakati wa tukio - Wapi:ni kiulizi cha mahali
- Vipi:kiulizi cha namna gani
Je ni neno la kuanzisha swali - Ngapi:kuuliza idadi kamili ya vitu , vyombo katika jumla
- Pi: kubainisha kati ya nyingi ili kupata kihusika au mhusika Fulani mahususi
Vielezi
Neno linaloeleza jinsi kitendo kilivyotendeka au kufafanua zaidi kuhusu kitendo
Aina za vielezi
- Wakati
- Namna
- Jinsi
- Mahali
- Idadi
- Vuhusishi
- Tanakali
- Takriri
- Tashbihi
Hutumika kwa - Lini- wakati
- Wapi – mahali
- Vipi – jinsi au namna
- Kiasi gani- idadi
Mifano
Wakati mahali namna
Leo nyumbani taratibu
Kesho darasani harakaharaka
Juma ijayo Nairobi ghafla
Mtondogoo machoni kivivu
Vielezi vya Mkazo
Takriri au shadda ni maneno yanayotumiwa kutilia mkazo au kusisitiza jambo
mifano ya takriri
- salama salimini
- bure bilashi
- raha na buraha
- kufa kupona
- liwalo liwe
- haambiliki hasemezeki
- fanya juu chini
- si wa uji si wa maji
- daima dawamu
- buheri wa afya
- hakubali hakatai
- hawashi hazimi
Ngeli pamoja Na Kirejeshi Amba
amba ni kitenzi kisaidizi kinachorejelea mtendwa au mtendaji kwa kutambulisha ama kueleza zaidi ya jambo fulani
kirejeshi –o hutumika badala ya AMBA
o-rejeshi na AMBA havitumiki pamoja
mfano
Kuku ambaye alitaga ni mkubwa
Nomino | Ngeli | Amba- | o-rejeshi |
Kuku |
A-WA |
Ambaye-ambao |
Ye-o Cho-vyo Lo-yo O-yo Yo-zo O-zo Yo-yo O-oO -yo Yo -yo Ko Po Ko MO |
Kirejeshi –amba
Kirejeshi –o cha awali na kirejessho o- cha tamati
Kufafanua jinsi ya kuambisha o rejeshi tamati na awali
o-rejeshi awali hutokea kabla ya mzizi wa kitenzi –o- rejeshi tamati hutokea mwishoni mwa sentensi
Kitenzi | o-rejeshi awali | o- rejeshi tamati |
Kimbia Kula Kuwa Kua |
Anayekimbia Anayekula Anayekuwa Anayekua |
Akimbiaye Alaye Awaye Akuwaye |
Matumizi ya –ndi
Kiainishi –ndi ni kishirikishi cha kukubali kwa msisitizo
Huambatanishwa na viwakilishi nafsi au virejeshi ili kutilia mkazo
Hutumia o-rejeshi kwenye vitenzi
Nafsi
Ndi + mimi = ndimi
Ndi + wewe = ndiwe
Ndi + yeye = ndiye
Ndi + si = ndisi
Ndi + nyinyi = ndinyi
Ndi + wao = ndio
o- rejeshi
ndi + ye = ndiye
ndi + o = ndio
Matumizi ya –si
Ni kiainishi cha kutilia mkazo
Huambatanishwa na viwakilishi nafsi au virejeshi ili kuleta msisitizo wa kukanusha
Nafsi
Si + mimi = simi
Si + wewe = siwe
Si + yeye = siye
Si + sisi = sisie
Si + wao = sio
o- Rejeshi
A –WA si + yeye = siye si + o = sio
KI – VI si + cho = sicho si+ vyo = sivyo
Matumizi ‘na’
Kiunganishi NA huambatanishwa na kiwakilishi nafsi kuonyesha PIA NA PAMOJA NA
Hutumiwa pamoja na 0-rejeshi
Nafsi
Ngeli Na + o- rejeshi
A – WA na+ye = naye nao
KI –VI na + cho = nacho navyo
LI –YA na + lo = nalo nayo
U – I na + o = nao nayo
U – ZI na + o = nao nazo
I – I na+ yo = nayo nayo
U – U na + o = nao nao
U – YA na + o= nao nayo
YA – YA na +yo = nayo nayo
I – ZI na + yo = nayo nazo
KU na + ko = nako
PAKUMU na+po na+ko na+mo
Matumizi ya ‘katika’, ‘ni’ , ‘kwenye’
Hivi ni vihusishi vya mahali
Hutumiwa kuonyesha kuwapo kwa kitu kilichotajwa mahali Fulani
Ngeli hubadilika hadi PA KU MU
Kuhimiza kuwa ni kosa kutumia hivi vihusishi pamoja
Kuambatanisha nomino na vivumishi
Vivumishi | Darasa | darasani |
Viashiria Vimilikishi Ote Oote Enyewe Enye Ingine Sifa |
Hili, hilo, lile Langu, lako,lake Lote Lolote Lenyewe Lenye Jingine Zuri, jema, baya Eupe, eusi Halina |
Hapa, hapo, pale |
Usemi Halisi na Taarifa
Usemi halisi ni maneno yalivyotarajiwa na msemaji mwenyewe
Usemi taarifa ni ripoti au maelezo yakitolewa na mtu mwengine kutoka kwa msemaji halisi
Kueleza jinsi ya kubadilisha usemi
Usemi halisi usemi taarifa
leo siku hiyo
Jana siku iliyopita/tangulia
Kesho siku ijayo
Viashiria hapa hapo au pale
Vimilikishi vya karibu ake
Mbali kidogo ako
Nafsi ya kwanza ni nafsi ya tatu
Wakati ta, ki nge
Mnyambuliko wa vitenzi
Kunyambua ni kurefusha mwisho wa vitenzi katika hali tofauti
- Tendeka
- Tendesha
- Tendeshwa
Katika kauli ya kutendeka vitenzi humalizika kwa ‘ka’
Kitenzi kauli ya kutendeka
Vuka vukika
Sahau sahaulika
Maliza malizika
Bomoa bomoka
Kula kulika
Lala lalika
Lima limika
Pika pikika
Soma someka
Fagia fagilika
Kitenzi tendesha kauli ya kutendeshwa
Lala laza lazwa
Pika pikisha pikishwa
Kimbia kimbiza kimbizwa
Rudi rudisha rudishwa
Toa toza tozwa
Ota otesha oteshwa
Oa oza ozwa
Soma somesha someshwa
Ukubwa na Udogo
Maneno katika hali ya ukubwa huwa ni kukipa kitu ukubwa usio wa kawaida na pia maneno katika hali ya udogo ni kukidunisha kitu kuliko hali ya kawaida
Ngeli pia hubadilika katika hali ya ukubwa na kuwa LI- YA ,na katika hali ya udogo huwa KI – VI
Njia tofauti za kubadili maneno katika ukubwa na udogo
Kudodosha – mw, ny na kutia j
Mfano
- ng’ombe – gombe
- Mkono – kono
- Ndama – dama
Kudodosha herufi moja na kutia ji
Mfano
- Mji – jiji
Kudodosha ki na kutia ji
Mfano
- Kisu – jisu
Kuongeza ji bila kudodoa chochote
Mfano
- Jicho – jijicho
Kutia j kwa nomino zinazoanza kwa irabu
Mfano
- uso – juso
- Uta – juta