0 votes
910 views
in Kigogo by
edited by

Mmesikia? Hamtatuletea wazimu wenu hapa! Nendeni kama mmekuja kutuhasimu.

  1. Eleza muktadha wa maneno. 
  2. Jadili umuhimu wa msemaji kwa hoja nne. 
  3. Fafanua mbinu ya lugha iliyotumika. 

1 Answer

0 votes
by

  1.    
    • Ni maneno ya Ngurumo 
    • Kwa Tunu 
    • Wakiwa Mangweni 
    • Asiya/ Mamapima alikuwa amekasirika baada ya mteja mmoja kuondoka na kuwafukuza akina Tunu kwa kuwapa dakika moja waondoke ndipo Ngurumo akauliza Tunu iwapo wamesikia kuwa waondoke wakiwa na Sudi. Tunu alikuwa amesema hapo mbeleni kuwa ni hatia kuuza pombe haramu na kuwa katiba imezifafanua sheria za uuzaji na unywaji pombe
  2.    
    •   (Ngurumo)
    • Anaendeleza maudhui ya ulevi; kijana anayejulikana kwa uraibu wa vileo
    • Anaendeleza maudhui ya taasubi ya kiume; kusema kuwa afadhali apigie paka kura kuliko mwamamke.
    • Anaendeleza maudhui ya uzinizu; kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mamapima ilhali ana mume.
    • Kielelezo cha usaliti ; anasaliti Wanasagamoyo kwa kuunga mkono uongozi dhalimu.
    • Anaonyesha ukatili wa Majoka; anauawa na chatu (kundi la Majoka) licha ya kuunga mkono utawala wa Majoka.
    • Anaonyesha ujinga wa Boza; Boza hagundui kuwa Boza ana uhusiano wa kimapenzi na mkewe licha ya kuwa mlevi mwenzake.
    • Kielelezo cha vijana ambao hawachangii katika maendeleo; anatumia wakati mwingi huko mangweni na hana mwelekeo.
  3.    

    • Kinaya; akina Tunu hawakuwa hasimu bali walitaka tu kuita watu kwa mkutano wa kusukuma viongozi wafungue soko na kuonyesha uvunjaji wa sheria katika kuuza pombe haramu.
    • kejeli; hamtatuletea wazimu wenu hapa. (yoyote moja)
Welcome to EasyElimu Questions and Answers, where you can ask questions and receive answers from other members of the community.

6.4k questions

9.6k answers

6 comments

590 users

...