Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Form 3 End Term 3 Exams 2023

Share via Whatsapp

MAAGIZO KWA MTAHINIWA:

  • Karatasi hii ina maswali manne.
  • Jibu maswali mawili pekee.Kila swali lina alama 20.
  • Swali la kwanza ni la lazima. kisha chagua swali la pili kutoka miongoni mwa matatu yaliyosalia.
  • Majibu yote yaandikwe katika lugha ya Kiswahili.
  1. Visa vingi vya udaganyifu katika mtihani wa kitaifa wa kuhitimu cheti cha sekondari vimekuwa vikiripotiwa nchini mwako kila uchao. Andika barua kwa mhariri kuhusu suala hili
  2. Serikali za magatuzi zitainua kiwango cha maendeleo nchini. Jadili.
  3. Tunga kisa kitakachodhihirisha maana ya methali: Mchagua nazi hupata koroma.
  4. Andika insha itakayoanza kwa maneno haya:
    Milipuko mikubwa ilisikika pu! Pu! Puu! Kisha niliwaona watu wakikimbia kuelekea pande zote…

                                                                           MWONGOZO WA KUSAHIHISHIA

  1. Hii ni insha ya kiuamilifu na kwa hivyo ina sura maalum. Hii insha iwe na kichwa mfano ifuate mtindo wa barua rasmi
    Sababu za udanganyifu kutokea, mfano
    1. Shinikizo kuwa wavyele wanataka wanao kupasi
    2. Ushindani baina ya shule mbalimbali
    3. Shinikizo la marafiki
    4. Walimu kutaka masomo yao kuongoza
    5. Shule kutaka hadhi ya shule kudumu
    6. Kutaka kupata nafasi ya digrii bora/kozi bora katika chuo kikuu
      Njia zinazowezesha udaganyifu
      • Matumizi ya rununu / simu
      • Wasimamizi wa mitihani kutomakinika
      • Ulegevu wa baraza la mitihani kwamba hapana mikakati madhubuti ya kukabiliana na udaganyifu
      • Kuwepo kwa mtandao na vitandazi vya kijamii kuwasiliana
        Mapendekezo
      • Baraza la mitihani kuwajibika
      • Adhabu kali kutolewa kwa wahusika
      • Kuwajibika kwa wasimamizi wa mitihani
      • Watahiniwa kufuzwa umuhimu wa kukwepa udaganyifu katika mitihani
  2. Serikali za magatuzi zitainua kiwango cha maendeleo nchini. Jadili.
    Zingatia baadhi ya hoja
    • Serikali zilizojikita mashinani
    • Huduma anuai zitapatikana karibu na wananchi
    • Mali ya asili itazalishwa pakubwa
    • Faida itatumika kuongeza / kuleta ushuru wa kaunti / gatuzi
    • Miundo msingi itaimarishwa sana
    • Ufisadi utapungua
    • Kila gatuzi litapania kuwa bora kimaendeleo
    • Umaskini utapunguka kwa kiasi kikubwa
    • Uzalendo utaimarika
  3. Mchagua nazi hupata koroma. Sharti aelewa kuwa ni methali.
    • Atunge kisa ambacho kinaoana vizuri na maana ya matumizi ya methali hii.
    • Kisa chake kiwe cha kuvutia.
    • Sharti aonyeshe pande mbili za methali.Aonyeshe mhusika anayechagua kitu au jambo zuri lakini analikosa na kupata lingine la kiwango cha chini.
    • Anatakiwa kuonyesha kuwa tusiwe watu wa kuchagua vitu bali tufanye bidii kupata tunachokihitaji.
  4. Andika insha itakayoanza kwa maneno haya:
    Milipuko mikubwa ilisikika pu! Pu! Puu! Kisha niliwaona watu wakikimbia kuelekea pande zote…
    • Ni sharti mtahiniwa aanze kwa maneno aliyopewa.
    • Anatakiwa kuanza kwa maneno yale bila ya kubadilisha wala kuyapunguza.
    • Kisa chake kiwa cha kuvutia na aonyeshe ni matukio yapi yaliyosababisha milipuko ile, kulikuwa na majeruhi na watu walitoroka kwenda wapi? Ni nini kilichotokea baada ya hapo?
    • Asipoanza kwa maneno aliyopewa atuzwe alama ya bakshishi
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Form 3 End Term 3 Exams 2023.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest